Psalms 91:1-4

Mungu Mlinzi Wetu


1 aYeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,
atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania.


2 cNitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”


3 dHakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji,
na maradhi ya kuambukiza ya kuua.

4 eAtakufunika kwa manyoya yake,
chini ya mbawa zake utapata kimbilio,
uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Copyright information for SwhKC